Ushirika wa Udiakonia Faraja

UMOJA WA UNDUGU WA WADIAKONIA.

Ushirika wa Diakonia Faraja ni Umoja wa Undugu wa Wadiakonia wa kiume na unamilikiwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Kaskazini. Wadiakonia ni watu wenye wito wa kweli na walioelimishwa na kubarikiwa kuwa watumishi katika huduma ya Diakonia katika Kanisa na jamii kwa ujumla. Kituo chetu kipo karibu na mji mdogo wa Sanya Juu, Wilaya ya Siha, Mkoa wa Kilimanjaro. Kwenye kituo hiki ndipo yalipo makao makuu ya Umoja wa Wadiakonia wote wa Dayosisi ya Kaskazini na ndipo mahali yanapotolewa mafunzo ya Udiakonia.

WADIAKONIA WANATUMIKA WAPI KATIKA KANISA.

Wadiakonia wanaweza kufanya kazi Sharikani, kwenye majimbo ya Dayosisi zetu na kwenye vituo vya Kanisa vinavyotoa huduma za Diakonia au vinavyohitaji taaluma aliyonayo Mdiakonia. Kwa kuwa na elimu ya Sekondari, mafunzo ya Udiakonia na elimu katika taaluma nyingine atakayokuwa nayo. Mdiakonia anaweza kufanyakazi kwenye vituo mbali mbali vya Kanisa mfano:Kuratibu huduma ya Diakonia ngazi ya jimbo katika Dayosisi zetu, Mdiakonia mwenye taaluma ya ualimu anaweza kufanyakazi katika shule za Kanisa kama mwalimu au Mkuu wa shule, Kama mratibu au msimamizi wa miradi ya Kanisa inayowahudumia Yatima , walemavu wa viungo, au walemavu wa akili, Watakaokuwa na taaluma ya afya ya binadamu wanaweza kufanyakazi katika vituo vya afya au hospitali za Kanisa, na watakaokuwa na taaluma ya uhasibu wanaweza kufanyakazi kama Wahasibu katika vituo mbali mbali vya Kanisa.

Our Mission

Mission Statement

To provide comprehensive care for people in mental, social or physical need, train young men to become Deacons of the ELCT/ND in order to enable them to support people in a professional way. To increase land for development of centers that trains young men to become Deacons and also establish economic projects for sustainability of the developed center; and provide Primary School Education for Physical handicapped children.

Our Vision

Vision Statement

To be Gods servants, who serve the Society, according to Christ’s words and deed, by providing good diaconal service in Tanzania.

Image Gallery

Services Overview

Ushirika wa Udiakonia Faraja Tunatoa huduma mbalimbali katika jamii ambayo imetuzunguka na kwa kanisa hasa kwa wale ambao walikuwa wamesahaulika katika jamii, Ndio maana tulianzisha shule ya msingi kwa watoto wenye ulemavu wa viungo.

Contact Us

Unaweza kutufikia kwa mawasiliano haya au kufika sanya juu mjini na kupanda Noah za karansi na kushuka kwa Mapadre.

Address:B.O.Box 167, Sanya Juu
Telephone: +255 755 807 199
Mobile: +255 766 515 319
Mobile: +255 757 618 508
E-mail: info@ushirika-wa-udiakonia-faraja.org

Imetengenezwa na Ushirika wa Udiakonia Faraja